Barker afurahia kuhamia KMC Complex

Joel JJ By Joel JJ • 12th May 2026


Barker afurahia kuhamia KMC Complex

Kocha Mkuu wa Simba SC, Steve Barker, ameeleza kufurahishwa na kiwango cha kikosi chake baada ya ushindi mnono wa mabao 4-0 dhidi ya Tanzania Prisons S.C. katika mchezo wa Ligi Kuu Tanzania Bara uliopigwa katika Uwanja wa KMC Complex.

Huo ulikuwa mchezo wa kwanza kwa Simba kutumia dimba hilo jipya tangu kuhamisha mechi zao za nyumbani kutoka Uwanja wa Meja Jenerali Isamuhyo, hatua ambayo imeonekana kuleta mabadiliko chanya kwa timu hiyo.

Akizungumza baada ya mchezo, Barker alisema ubora wa uwanja wa KMC Complex umewasaidia wachezaji wake kutekeleza vyema mbinu za mchezo, huku akisisitiza kuwa kikosi chake kinaendelea kuelewa falsafa yake ya ufundishaji.

Alisema:

“Tulicheza kwenye uwanja mzuri ambao haukuwa na matuta mengi, hivyo hilo lilitusaidia sana. Tulianza mchezo vizuri, tukautawala kwa nguvu na intensiti ya juu.”

Kocha huyo aliongeza kuwa mabao waliyofunga yalikuwa matokeo ya uchezaji mzuri na wa kushirikiana, huku Simba wakiwazuia wapinzani wao kupata nafasi za hatari.

“Tulipofunga mabao yetu, yalikuwa ya kustahili kutokana na namna tulivyocheza. Tulidhibiti mchezo na kuwafanya wapinzani washindwe kupata nafasi,” alisema Barker.

Hata hivyo, alisema licha ya ushindi mkubwa, bado anaangalia ratiba ngumu iliyo mbele ya timu yake, akibainisha umuhimu wa usimamizi wa nguvu za wachezaji kutokana na michezo mingi mfululizo.

“Wakati mwingine unataka mabao mengi zaidi, lakini lazima usimamie nguvu. Tuna mechi nyingi ndani ya siku chache zijazo, hivyo tulihitaji kuwa makini,” aliongeza.

Baada ya ushindi huo, Simba inaelekea mkoani Kigoma kucheza dhidi ya Mashujaa FC katika Uwanja wa Lake Tanganyika, kabla ya kurejea Dar es Salaam kwa mchezo wa robo fainali ya Kombe la CRDB dhidi ya TRA United.


  

More Stories

Azam Fc hiyooo fainali, yaichapa Yanga 3-2 nusu fainali
Azam Fc hiyooo fainali, yaichapa Yanga 3-2 nusu fainali
Today, READ MORE →
Azam Fc 3-2 Yanga, CRDB Cup
Azam Fc 3-2 Yanga, CRDB Cup
Today, READ MORE →
Ni Azam Fc vs Yanga, nani anakwenda fainali kombe la CRDB?
Ni Azam Fc vs Yanga, nani anakwenda fainali kombe la CRDB?
Today, READ MORE →
Liverpool kuongeza dau kumnasa Diomande
Liverpool kuongeza dau kumnasa Diomande
Today, READ MORE →
Prisons wamefufua matumaini kusalia ligi kuu
Prisons wamefufua matumaini kusalia ligi kuu
Today, READ MORE →
Tunisia yaaga kombe la Dunia kwa aibu, yapigwa 4-0 na Japan
Tunisia yaaga kombe la Dunia kwa aibu, yapigwa 4-0 na Japan
Today, READ MORE →
Ivory Coast yapoteza dhidi ya Ujerumani dakika za jioni
Ivory Coast yapoteza dhidi ya Ujerumani dakika za jioni
Today, READ MORE →
Real Madrid yakana kuwasiliana na Olise, wakala wake
Real Madrid yakana kuwasiliana na Olise, wakala wake
Yesterday, READ MORE →
Simba 4-0 Coastal Union, CRDB Cup
Simba 4-0 Coastal Union, CRDB Cup
Yesterday, READ MORE →
Simba yaifumua Coastal Union 4-0, yatinga fainali ya CRDB Bank Cup
Simba yaifumua Coastal Union 4-0, yatinga fainali ya CRDB Bank Cup
Yesterday, READ MORE →