International,Transfer News,Kaize Chiefs

Da Cruz Kocha Mpya Kaizer Chiefs

Joel JJ By Joel JJ
β€’
1 Jun 2026
Da Cruz Kocha Mpya Kaizer Chiefs

Klabu ya Kaize Chiefs ya Afrika Kusini, imemteua kocha Mfaransa, Fernando Da Cruz, kuwa meneja mkuu wa timu hiyo kwa mkataba wa miaka miwili, huku kukiwa na kipengele cha kuongeza mwaka mmoja zaidi.

Kwa mujibu wa taarifa za karibu na klabu, Da Cruz amekamilisha makubaliano na uongozi wa Kaizer Chiefs na kusaini mkataba huo mpya unaomuweka rasmi kama mrithi wa majukumu ya kuiongoza timu hiyo katika msimu ujao.

Kocha huyo wa zamani wa Lille OSC na pia aliyewahi kufanya kazi na AS FAR Rabat, anatarajiwa kuwasili akiwa na timu yake ya wasaidizi wanne, huku pia wakiunganishwa na makocha 2–3 wa Afrika Kusini ili kusaidia mchakato wa ujenzi wa kikosi.

Uongozi wa Kaizer Chiefs umeonekana kuwa katika hatua ya kujenga upya timu ili kurudisha makali yao kwenye ligi ya Afrika Kusini baada ya misimu ya matokeo yasiyoridhisha.

Ujio wa Da Cruz unaashiria mwelekeo mpya wa kimkakati, ambapo klabu hiyo inatarajia kutumia uzoefu wake wa kimataifa kuimarisha nidhamu ya kiufundi, mbinu za kisasa za soka na ushindani katika ligi na mashindano ya Kimaataifa.

Msimu uliopita Chiefs ilinolewa na makocha vijana Cedric Kaze na Ben Youssef ambao walichukua majukumu yaliyoachwa na aliyekuwa kocha mkuu Nasreddine Nabi ambaye aliondoka kutokana na changamoto za kifamilia.

More Stories

Nyota Geita Gold afunguka rafu ya Aziz KI, Ilikuwa bahati mbaya
Nyota Geita Gold afunguka rafu ya Aziz KI, Ilikuwa bahati mbaya
1h ago
READ MORE β†’
LAPORTA: Atletico kumuuza Alvarez kwa timu yeyote isipokuwa Barcelona
LAPORTA: Atletico kumuuza Alvarez kwa timu yeyote isipokuwa Barcelona
3h ago
READ MORE β†’
Ngorongoro Heroes yatangulia nusu fainali CECAFA U20 kwa kishindo
Ngorongoro Heroes yatangulia nusu fainali CECAFA U20 kwa kishindo
5h ago
READ MORE β†’
Samatta afunga bao lake la pili, Le Havre ikipoteza
Samatta afunga bao lake la pili, Le Havre ikipoteza
5h ago
READ MORE β†’
Salah hakamatiki Uturuki, apiga hat-trik Trabzonspor ikiifumua Galatasaray 4-0
Salah hakamatiki Uturuki, apiga hat-trik Trabzonspor ikiifumua Galatasaray 4-0
6h ago
READ MORE β†’
Azam Fc yaonywa, Yanga yakumbana na faini - Kamati ya saa 72
Azam Fc yaonywa, Yanga yakumbana na faini - Kamati ya saa 72
6h ago
READ MORE β†’
Mshambuliaji wa zamani Yanga aibukia Zambia
Mshambuliaji wa zamani Yanga aibukia Zambia
7h ago
READ MORE β†’
Barcelona yaendeleza kichapo Laliga ikimfunga Sevilla, Raphinha hashikiki.
Barcelona yaendeleza kichapo Laliga ikimfunga Sevilla, Raphinha hashikiki.
14h ago
READ MORE β†’
Mamelodi Sundowns yaibuka kidedea mbele ya Al Ahli
Mamelodi Sundowns yaibuka kidedea mbele ya Al Ahli
19h ago
READ MORE β†’
Arsenal yaduwazwa 3-0 na Brighton
Arsenal yaduwazwa 3-0 na Brighton
19h ago
READ MORE β†’