Da Cruz Kocha Mpya Kaizer Chiefs

Joel JJ By Joel JJ β€’ 1st June 2026


Da Cruz Kocha Mpya Kaizer Chiefs

Klabu ya Kaize Chiefs ya Afrika Kusini, imemteua kocha Mfaransa, Fernando Da Cruz, kuwa meneja mkuu wa timu hiyo kwa mkataba wa miaka miwili, huku kukiwa na kipengele cha kuongeza mwaka mmoja zaidi.

Kwa mujibu wa taarifa za karibu na klabu, Da Cruz amekamilisha makubaliano na uongozi wa Kaizer Chiefs na kusaini mkataba huo mpya unaomuweka rasmi kama mrithi wa majukumu ya kuiongoza timu hiyo katika msimu ujao.

Kocha huyo wa zamani wa Lille OSC na pia aliyewahi kufanya kazi na AS FAR Rabat, anatarajiwa kuwasili akiwa na timu yake ya wasaidizi wanne, huku pia wakiunganishwa na makocha 2–3 wa Afrika Kusini ili kusaidia mchakato wa ujenzi wa kikosi.

Uongozi wa Kaizer Chiefs umeonekana kuwa katika hatua ya kujenga upya timu ili kurudisha makali yao kwenye ligi ya Afrika Kusini baada ya misimu ya matokeo yasiyoridhisha.

Ujio wa Da Cruz unaashiria mwelekeo mpya wa kimkakati, ambapo klabu hiyo inatarajia kutumia uzoefu wake wa kimataifa kuimarisha nidhamu ya kiufundi, mbinu za kisasa za soka na ushindani katika ligi na mashindano ya Kimaataifa.

Msimu uliopita Chiefs ilinolewa na makocha vijana Cedric Kaze na Ben Youssef ambao walichukua majukumu yaliyoachwa na aliyekuwa kocha mkuu Nasreddine Nabi ambaye aliondoka kutokana na changamoto za kifamilia.


  

More Stories

Azam Fc hiyooo fainali, yaichapa Yanga 3-2 nusu fainali
Azam Fc hiyooo fainali, yaichapa Yanga 3-2 nusu fainali
Today, READ MORE β†’
Azam Fc 3-2 Yanga, CRDB Cup
Azam Fc 3-2 Yanga, CRDB Cup
Today, READ MORE β†’
Ni Azam Fc vs Yanga, nani anakwenda fainali kombe la CRDB?
Ni Azam Fc vs Yanga, nani anakwenda fainali kombe la CRDB?
Today, READ MORE β†’
Liverpool kuongeza dau kumnasa Diomande
Liverpool kuongeza dau kumnasa Diomande
Today, READ MORE β†’
Prisons wamefufua matumaini kusalia ligi kuu
Prisons wamefufua matumaini kusalia ligi kuu
Today, READ MORE β†’
Tunisia yaaga kombe la Dunia kwa aibu, yapigwa 4-0 na Japan
Tunisia yaaga kombe la Dunia kwa aibu, yapigwa 4-0 na Japan
Today, READ MORE β†’
Ivory Coast yapoteza dhidi ya Ujerumani dakika za jioni
Ivory Coast yapoteza dhidi ya Ujerumani dakika za jioni
Today, READ MORE β†’
Real Madrid yakana kuwasiliana na Olise, wakala wake
Real Madrid yakana kuwasiliana na Olise, wakala wake
Yesterday, READ MORE β†’
Simba 4-0 Coastal Union, CRDB Cup
Simba 4-0 Coastal Union, CRDB Cup
Yesterday, READ MORE β†’
Simba yaifumua Coastal Union 4-0, yatinga fainali ya CRDB Bank Cup
Simba yaifumua Coastal Union 4-0, yatinga fainali ya CRDB Bank Cup
Yesterday, READ MORE β†’