International,Normal News,Raja CA, Yanga, Local

Nabi kurithi mikoba ya Fadlu Davis Raja CA

Joel JJ By Joel JJ
β€’
12 Jun 2026
Nabi kurithi mikoba ya Fadlu Davis Raja CA

Kocha wa zamani wa Kaizer Chiefs, Nasreddine Nabi, anatarajiwa kutua jijini Casablanca kwa ajili ya kukamilisha taratibu za mwisho za kujiunga na Raja Club Athletic (Raja CA).

Kwa mujibu wa taarifa, Nabi na Raja CA tayari wamefikia makubaliano ya awali kuhusu mkataba utakaoendelea hadi mwisho wa msimu ujao, huku masuala madogo ya kiutawala yakisalia kabla ya tangazo rasmi kutolewa.

Kocha huyo raia wa Tunisia atachukua nafasi ya Fadlu Davids kwenye benchi la ufundi la miamba hiyo ya Morocco. Raja imekuwa ikimfuatilia Nabi kwa muda mrefu kutokana na rekodi yake nzuri katika soka la Afrika na uzoefu wake mkubwa ndani ya ukanda wa Afrika Kaskazini.

Nabi ni jina linalofahamika sana kwa mashabiki wa soka Afrika Mashariki baada ya mafanikio makubwa aliyoyapata akiwa kocha wa Yanga, ambapo aliiongoza klabu hiyo kutwaa mataji mawili mfululizo ya Ligi Kuu Tanzania Bara pamoja na kufika fainali ya Kombe la Shirikisho Afrika mwaka 2023. Baadaye alihamia AS FAR ya Morocco kabla ya kujiunga na Kaizer Chiefs ya Afrika Kusini mwaka 2024.

Ingawa kipindi chake Kaizer Chiefs kilikumbwa na changamoto mbalimbali, Nabi aliweza kuiongoza timu hiyo kutwaa Nedbank Cup na kumaliza ukame wa miaka kadhaa bila taji, jambo lililoendelea kuimarisha hadhi yake kama mmoja wa makocha wanaoheshimika barani Afrika.

More Stories

Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
45m ago
READ MORE β†’
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
1h ago
READ MORE β†’
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
1h ago
READ MORE β†’
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
2h ago
READ MORE β†’
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
3h ago
READ MORE β†’
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
4h ago
READ MORE β†’
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
4h ago
READ MORE β†’
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
17h ago
READ MORE β†’
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
17h ago
READ MORE β†’
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
18h ago
READ MORE β†’