Local,Normal News,Prisons

Prisons wamefufua matumaini kusalia ligi kuu

Joel JJ By Joel JJ
β€’
21 Jun 2026
Prisons wamefufua matumaini kusalia ligi kuu

Klabu ya Tanzania Prisons, imeanza kuandika upya simulizi yao kwenye Ligi Kuu Tanzania Bara baada ya kupata mfululizo wa matokeo chanya yaliyoibua matumaini mapya ya kusalia kwenye ligi hiyo msimu huu.

Baada ya mwanzo mbaya ulioifanya timu hiyo kupitia kipindi kigumu kilichoshuhudia uongozi ukifanya mabadiliko ya benchi la ufundi, sasa mwanga unaanza kuonekana ndani ya kikosi hicho cha Jeshi la Magereza. Ushindi wa mechi tatu mfululizo umebadilisha kabisa hali ya hewa kambini na kurejesha imani kwa mashabiki.

Katika michezo yao ya karibuni, Tanzania Prisons imeonyesha uimara mpya. Kwanza waliibuka na ushindi wa mabao 3-2 ugenini Mwanza, kisha wakarejea Uwanja wa Sokoine na kuifunga Dodoma Jiji mabao 3-1, kabla ya kumalizia mfululizo huo kwa ushindi wa bao 1-0 dhidi ya JKT Tanzania.

Matokeo hayo yameiwezesha Prisons kupanda hadi nafasi ya 14 kwenye msimamo wa ligi wakiwa na pointi 26, hatua inayowapa nafasi ya kupigania kubaki salama msimu huu badala ya kuangukia kwenye presha ya kucheza mechi za mchujo.

Kwa sasa, kikosi hicho kina mechi tatu muhimu zilizobaki ambazo zinaweza kuamua kabisa hatma yao ya ligi. Wanatarajiwa kuanza dhidi ya Singida Black Stars Juni 24 mjini Singida, kabla ya kurejea Mbeya kumenyana na Mtibwa Sugar, na baadaye kumalizia ugenini dhidi ya Mashujaa FC.

Mchezo dhidi ya Singida Black Stars unaonekana kuwa wa β€œmaamuzi mapema,” ukizingatiwa ushindani wa alama ulivyo karibu katika sehemu ya chini ya msimamo.

Nahodha wa Tanzania Prisons, Lambart Sabiyanka, amekiri wazi kuwa hali ya timu sasa ni tofauti na ilivyokuwa mwanzo wa msimu. Kwa mujibu wake, ushindi huo umeongeza morali na umoja ndani ya kikosi.

Amesema mchezo dhidi ya Singida Black Stars una nafasi kubwa ya kuamua mwelekeo wa Prisons kwenye msimu huu, akisisitiza kuwa lengo lao ni kuepuka kabisa mashindano ya mchujo wa kushuka daraja.

β€œSingida Black Stars wameshikilia pakubwa hatma yetu. Tukivuka salama tunaweza kupata nafuu kubwa,” amesema Sabiyanka.

Ameongeza kuwa kila mchezaji sasa anapigania nembo ya klabu hiyo kwa bidii kubwa, huku akisisitiza umuhimu wa kucheza kwa tahadhari na hesabu sahihi katika mechi zilizobaki.

More Stories

Barcelona yaendeleza kichapo Laliga ikimfunga Sevilla, Raphinha hashikiki.
Barcelona yaendeleza kichapo Laliga ikimfunga Sevilla, Raphinha hashikiki.
2h ago
READ MORE β†’
Mamelodi Sundowns yaibuka kidedea mbele ya Al Ahli
Mamelodi Sundowns yaibuka kidedea mbele ya Al Ahli
6h ago
READ MORE β†’
Arsenal yaduwazwa 3-0 na Brighton
Arsenal yaduwazwa 3-0 na Brighton
7h ago
READ MORE β†’
Nyota Stars waingia kambini tayari kwa mechi za kufuzu Afcon 2027
Nyota Stars waingia kambini tayari kwa mechi za kufuzu Afcon 2027
9h ago
READ MORE β†’
Simba kujichimbia Afrika Kusini kujiandaa na Kariakoo Derby
Simba kujichimbia Afrika Kusini kujiandaa na Kariakoo Derby
9h ago
READ MORE β†’
Madrid Derby: Atletico na Real kwenye vita ya majirani
Madrid Derby: Atletico na Real kwenye vita ya majirani
13h ago
READ MORE β†’
Hii hapa rekodi tamu ya Barker Ligi Kuu
Hii hapa rekodi tamu ya Barker Ligi Kuu
15h ago
READ MORE β†’
Sundowns kuchuana na Al Ahli katika vita ya Afrika na Asia
Sundowns kuchuana na Al Ahli katika vita ya Afrika na Asia
15h ago
READ MORE β†’
Ft: Yanga 1-0 St George, Yanga yapata ushindi mechi ya kirafiki.
Ft: Yanga 1-0 St George, Yanga yapata ushindi mechi ya kirafiki.
1d ago
READ MORE β†’
Dockers Derby yarudi baada ya miaka 14, Ulinzi wa London ukiimarishwa.
Dockers Derby yarudi baada ya miaka 14, Ulinzi wa London ukiimarishwa.
1d ago
READ MORE β†’