Yanga yawasiliana na Fadlu Davids

Joel JJ By Joel JJ β€’ 28th June 2026


Yanga yawasiliana na Fadlu Davids

Vyanzo vya kuaminika vinaeleza kuwa klabu ya Yanga SC imeanza mazungumzo ya awali na aliyekuwa kocha wa Raja Casablanca, Fadlu Davids, kuhusu uwezekano wa kuchukua nafasi ya ukocha mkuu wa mabingwa hao wa kihistoria.

Taarifa hizo zinaeleza kuwa uongozi wa Yanga umemvutia sana kocha huyo raia wa Afrika Kusini kutokana na rekodi yake ya mafanikio katika klabu mbalimbali barani Afrika, ikiwemo kuiboresha Simba SC na kuifikisha fainali ya Kombe la Shirikisho Afrika (CAF Confederation Cup).

Fadlu aliondoka Raja Casablanca hivi karibuni kwa makubaliano ya pande zote mbili baada ya timu hiyo kupoteza michezo miwili mfululizo katika Ligi Kuu ya Morocco na kupoteza matumaini ya kutwaa ubingwa.

Inaelezwa pia kuwa Yanga imekuwa ikimfuatilia kocha huyo kwa muda, hasa kutokana na uwezo wake wa kujenga timu zenye nidhamu ya kiufundi na uwezo wa kushindana kimataifa, jambo lililoonekana wazi alipokuwa Simba SC ambapo aliwafanya Wekundu hao wa Msimbazi kufanya vizuri kwenye mashindano ya CAF.

Kwa sasa, taarifa zinaeleza kuwa mazungumzo bado yako katika hatua za awali, huku pande zote mbili zikijadiliana masharti kabla ya kufikia makubaliano yoyote rasmi. Hata hivyo, dalili zinaonyesha kuwa kocha huyo yuko tayari kujiunga na Yanga endapo makubaliano yatakamilika.

Kwa sasa Yanga inanolewa na kocha Abdihamid Moalin baada ya kuachana na Pedro Goncalves raia wa Ureno


  

More Stories

Canada waiondoa Bafana bafana dakika za jioni, Watinga 16 bora kwa mara ya kwanza
Canada waiondoa Bafana bafana dakika za jioni, Watinga 16 bora kwa mara ya kwanza
Today, READ MORE β†’
Afrika Kusini na Canada kufungua 32 bora leo
Afrika Kusini na Canada kufungua 32 bora leo
Today, READ MORE β†’
Yanga yawasiliana na Fadlu Davids
Yanga yawasiliana na Fadlu Davids
Today, READ MORE β†’
Hatua ya Makundi  Kombe la Dunia 2026 Yahitimishwa,  32 Bora Kuanza Leo
Hatua ya Makundi Kombe la Dunia 2026 Yahitimishwa, 32 Bora Kuanza Leo
Today, READ MORE β†’
Messi kashindikana! afunga bao la sita, Argentina ikiichapa Jordan 3-1
Messi kashindikana! afunga bao la sita, Argentina ikiichapa Jordan 3-1
Today, READ MORE β†’
Mayele atupia DR Congo ikiweka rekodi ya kufuzu 32 bora kombe la Dunia
Mayele atupia DR Congo ikiweka rekodi ya kufuzu 32 bora kombe la Dunia
Today, READ MORE β†’
Uingereza yafuzu kibabe kundi L, yamaliza kwa ushindi wa 2-0 dhidi ya Panama
Uingereza yafuzu kibabe kundi L, yamaliza kwa ushindi wa 2-0 dhidi ya Panama
Today, READ MORE β†’
Licha ya kipigo dhidi ya Croatia, Ghana yafuzu 32 bora
Licha ya kipigo dhidi ya Croatia, Ghana yafuzu 32 bora
Today, READ MORE β†’
Yanga, Simba zachuana kwenye ubingwa hadi mwisho
Yanga, Simba zachuana kwenye ubingwa hadi mwisho
Yesterday, READ MORE β†’
Misri yatinga hatua ya 32 Bora baada ya sare dhidi ya Iran
Misri yatinga hatua ya 32 Bora baada ya sare dhidi ya Iran
Yesterday, READ MORE β†’