Ligi Kuu ya NBC inahitimishwa kesho Jumanne kwa timu zote 16 kushuka viwanjani kucheza mechi za mwisho wa msimu.
Ukiacha vita ya Yanga na Simba kwenye ubingwa na vita ya chini ya msimamo wa ligi, kuna hii vita ya kuwania ufungaji bora.
Feisal Salum wa Azam Fc, Allan Okello wa Yanga na Ndumumwe Mossi wa Singida BS wanachuana vikali kuwania kiatu cha ufungaji bora.
Fei Toto anaongoza akiwa na mabao 15 wakati Okello na Mossi kila mmoja amefunga mabao 14.
Lakini kwa karibu wanafuatiwa na Mathew Tegis wa Pamba Jiji mwenye mabao 11 sawa na Fabrice Ngoy wa Namungo Fc.
Fei Toto atakamilisha mechi ya mwisho nyumbani dhidi ya Dodoma Jiji, wakati Okello na Mossi watakuwa ugenini.
Okello atakuwa dimba la Meja Jenerali Isamuhyo wakati Yanga ikichuana na JKT Tanzania wakati Mossi atakuwa Arusha dimba la Sheikh Amri Abeid Singida BS ikichuana na Fountain Gate.




