Baada ya kumalizika kwa msimu wa Ligi Kuu ya NBC, uongozi wa Simba umeelekeza nguvu zote kwenye mchezo wa fainali ya Kombe la CRDB, ukilenga kumaliza msimu kwa kutwaa taji hilo.
Meneja wa Habari na Mawasiliano wa Simba, Ahmed Ali, amesema wachezaji, benchi la ufundi na viongozi wote wamejipanga kuhakikisha wanaleta furaha kwa mashabiki kwa kushinda fainali dhidi ya Azam FC.





