Klabu ya JKT Tanzania imemuongeza mkataba wa miaka miwili kocha wake mkuu Ahmed Ally. Baada ya kuwaongoza maafande hao msimu uliomalizika kumaliza nafasi ya 6, mabosi wa JKT Tanzania wameridhika na kazi yake na sasa wamemkabidhi timu hadi mwaka 2028.
JKT Tanzania ni moja ya timu zilizokuwa tishio msimu uliomalizika ikifanikiwa kushinda mechi 10, sare 12 na kutoka sare mechi nane wakimaliza msimu na alama 42. Kuna nyakati maafande hao walikaa kileleni mwa msimamo wa ligi kwa wiki kadhaa.
Ahmed Ally ni miongoni mwa makocha vijana wazawa ambao wameendelea kudhihirisha kuwa hata makocha wa ndani wakiaminiwa wanaweza.
Ahmed yuko sehemu ya benchi la ufundi la timu ya Taifa ya Tanzania 'Taifa Stars' inayonolewa na kocha Miguel Gamondi



