Mahrez astaafu kutumikia Algeria , Baada ya Taifa ilo Kuondoshwa Kombe la dunia

Abdulrahman Said By Abdulrahman Said β€’ 3rd July 2026


Mahrez astaafu kutumikia Algeria , Baada ya Taifa ilo Kuondoshwa Kombe la dunia

Nahodha wa Algeria, Riyad Mahrez, ametangaza kustaafu rasmi soka la kimataifa baada ya timu yake kuaga Kombe la Dunia 2026 kufuatia kichapo cha mabao 2-0 dhidi ya Uswisi katika hatua ya 32 Bora. Matokeo hayo yaliihakikishia Uswisi tiketi ya kutinga hatua ya 16 Bora, huku yakihitimisha safari ya Algeria kwenye mashindano hayo.

Katika mchezo huo uliochezwa jijini Vancouver, Breel Embolo aliifungia Uswisi bao la kwanza katika dakika ya 10 kabla ya Dan Ndoye kuongeza la pili mwanzoni mwa kipindi cha pili. Licha ya juhudi za Algeria kutafuta njia ya kurejea mchezoni, walishindwa kupenya safu imara ya ulinzi ya wapinzani wao.

Akizungumza baada ya mchezo, Mahrez alithibitisha kuwa hiyo ilikuwa mechi yake ya mwisho akiwa na jezi ya timu ya taifa ya Algeria. Nyota huyo anastaafu akiwa ameichezea nchi yake mechi 119, akifunga mabao 40 na kutoa pasi za mabao 45, rekodi inayomweka miongoni mwa wachezaji walioitumikia Algeria kwa mafanikio makubwa zaidi.

Katika kipindi chake cha kuitumikia Algeria, Mahrez ameandika historia kwa kuiongoza timu hiyo kutwaa Kombe la Mataifa ya Afrika (AFCON) mwaka 2019, mafanikio yaliyorejesha heshima ya soka la taifa hilo barani Afrika. Mbali na kutwaa tuzo ya Mchezaji Bora wa Afrika mwaka 2016, amemaliza maisha yake ya kimataifa akiwa ameichezea Algeria mechi 119, akifunga mabao 40 na kutoa pasi za mabao 45, rekodi zinazomweka miongoni mwa wachezaji wakubwa na wenye mafanikio makubwa zaidi katika historia ya soka la Algeria.


  

More Stories

Man United waingia kwenye mazungumzo na winga wa West Ham, wakiendelea kupush kwa Baleba pia.
Man United waingia kwenye mazungumzo na winga wa West Ham, wakiendelea kupush kwa Baleba pia.
Today, READ MORE β†’
Simba waifuata Azam kibabe
Simba waifuata Azam kibabe
Today, READ MORE β†’
Mahrez astaafu kutumikia Algeria , Baada ya Taifa ilo Kuondoshwa Kombe la dunia
Mahrez astaafu kutumikia Algeria , Baada ya Taifa ilo Kuondoshwa Kombe la dunia
Today, READ MORE β†’
Ureno yaokoka kwa chupuchupu, yatinga16 bora baada ya kuitoa Croatia 2-1
Ureno yaokoka kwa chupuchupu, yatinga16 bora baada ya kuitoa Croatia 2-1
Today, READ MORE β†’
Algeria yaaga kombe la Dunia, yapigwa 2-0 na Uswisi
Algeria yaaga kombe la Dunia, yapigwa 2-0 na Uswisi
Today, READ MORE β†’
Klopp kumrithi Nagelsmann Ujerumani
Klopp kumrithi Nagelsmann Ujerumani
Today, READ MORE β†’
Spain wafanikiwa kutinga Hatua ya 16 Bora WC26 Kibabe.
Spain wafanikiwa kutinga Hatua ya 16 Bora WC26 Kibabe.
Today, READ MORE β†’
Yanga yapata pigo lingine
Yanga yapata pigo lingine
Today, READ MORE β†’
Dube Aikacha Yanga na Kurejea Kwao Zimbabwe
Dube Aikacha Yanga na Kurejea Kwao Zimbabwe
Today, READ MORE β†’
Mouringo ampeleka Camavinga Man City
Mouringo ampeleka Camavinga Man City
Yesterday, READ MORE β†’