Nahodha wa Algeria, Riyad Mahrez, ametangaza kustaafu rasmi soka la kimataifa baada ya timu yake kuaga Kombe la Dunia 2026 kufuatia kichapo cha mabao 2-0 dhidi ya Uswisi katika hatua ya 32 Bora. Matokeo hayo yaliihakikishia Uswisi tiketi ya kutinga hatua ya 16 Bora, huku yakihitimisha safari ya Algeria kwenye mashindano hayo.
Katika mchezo huo uliochezwa jijini Vancouver, Breel Embolo aliifungia Uswisi bao la kwanza katika dakika ya 10 kabla ya Dan Ndoye kuongeza la pili mwanzoni mwa kipindi cha pili. Licha ya juhudi za Algeria kutafuta njia ya kurejea mchezoni, walishindwa kupenya safu imara ya ulinzi ya wapinzani wao.
Akizungumza baada ya mchezo, Mahrez alithibitisha kuwa hiyo ilikuwa mechi yake ya mwisho akiwa na jezi ya timu ya taifa ya Algeria. Nyota huyo anastaafu akiwa ameichezea nchi yake mechi 119, akifunga mabao 40 na kutoa pasi za mabao 45, rekodi inayomweka miongoni mwa wachezaji walioitumikia Algeria kwa mafanikio makubwa zaidi.
Katika kipindi chake cha kuitumikia Algeria, Mahrez ameandika historia kwa kuiongoza timu hiyo kutwaa Kombe la Mataifa ya Afrika (AFCON) mwaka 2019, mafanikio yaliyorejesha heshima ya soka la taifa hilo barani Afrika. Mbali na kutwaa tuzo ya Mchezaji Bora wa Afrika mwaka 2016, amemaliza maisha yake ya kimataifa akiwa ameichezea Algeria mechi 119, akifunga mabao 40 na kutoa pasi za mabao 45, rekodi zinazomweka miongoni mwa wachezaji wakubwa na wenye mafanikio makubwa zaidi katika historia ya soka la Algeria.



