Local,Normal News,Azam, Simba, Yanga, Kipre Jr, NBC LEAGUE

Rasmi Kipre Jr arejea Azam fc

Abdulrahman Said By Abdulrahman Said
15 Jul 2026
Rasmi Kipre Jr arejea Azam fc

Klabu ya Azam FC imethibitisha rasmi kurejea kwa kiungo mshambuliaji wa Ivory Coast, Zunon Kipré Emmanuel Junior maarufu kama Kipre Junior, baada ya kufikia makubaliano ya uhamisho na MC Alger ya Algeria. Nyota huyo amesaini mkataba na kutambulishwa rasmi katika makao makuu ya klabu, akirejea Chamazi baada ya kuondoka mwaka 2024.

Kipre alijiunga na MC Alger mwaka 2024 kwa dau lililoripotiwa kuzidi Shilingi milioni 700, ambapo aliisaidia klabu hiyo kutwaa mataji mawili ya Ligi Kuu ya Algeria pamoja na Kombe la Super la Algeria. Hata hivyo, baada ya misimu miwili nchini humo, pande zote mbili zilikubaliana kuvunja mkataba wake, hatua iliyofungua njia ya kurejea Azam FC.

Kwa mujibu wa makubaliano ya uhamisho huo, MC Alger itabaki na asilimia 30 ya ada ya mauzo ya baadaye endapo Azam FC itaamua kumuuza mchezaji huyo kwa klabu nyingine. Kurejea kwake kunatarajiwa kuimarisha safu ya ushambuliaji ya Azam FC kuelekea msimu wa 2026/27.

Katika kipindi chake cha kwanza akiwa Azam FC, Kipre Junior alicheza misimu miwili na kufunga mabao 12, akijijengea sifa kwa ubunifu, kasi na uwezo wake wa kutengeneza nafasi za mabao. Mashabiki wa Azam FC sasa wanatarajia kurejea kwake kutakuwa chachu ya mafanikio mapya huku klabu hiyo ikijiandaa kwa ushindani wa msimu mpya wa Ligi Kuu Tanzania Bara na mashindano mengine.

More Stories

APR Fc yawaondosha aigles du congo kwenye caf champions league
APR Fc yawaondosha aigles du congo kwenye caf champions league
4h ago
READ MORE →
Azam Fc yaomboleza kifo cha mlinda lango U20
Azam Fc yaomboleza kifo cha mlinda lango U20
8h ago
READ MORE →
Hatuna presha kuikabili Yanga - Kocha Gaborone United
Hatuna presha kuikabili Yanga - Kocha Gaborone United
10h ago
READ MORE →
Manqoba aweka tahadhari mechi dhidi ya Gaborone United
Manqoba aweka tahadhari mechi dhidi ya Gaborone United
12h ago
READ MORE →
Rasmi: João Pedro Atwaa Tuzo Ya Mchezaji Bora Wa Mwezi Wa Agosti
Rasmi: João Pedro Atwaa Tuzo Ya Mchezaji Bora Wa Mwezi Wa Agosti
14h ago
READ MORE →
Simba inalenga hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, nusu fainali ni lengo kubwa
Simba inalenga hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, nusu fainali ni lengo kubwa
14h ago
READ MORE →
Libasse awapiga chini Max na Mwajanga, Kwenye tuzo za Mwezi.
Libasse awapiga chini Max na Mwajanga, Kwenye tuzo za Mwezi.
14h ago
READ MORE →
Fei Toto azipotezea Simba, Yanga
Fei Toto azipotezea Simba, Yanga
16h ago
READ MORE →
Xtra 90 Bets : Utabiri wa mechi 21, Septemba 11 2026
Xtra 90 Bets : Utabiri wa mechi 21, Septemba 11 2026
20h ago
READ MORE →
UEFA champions league: matokeo ya usiku
UEFA champions league: matokeo ya usiku
1d ago
READ MORE →