International,Normal News,Yanga sc, Mamelodi Sundowns, Orlando pirates

‘Waziri wa Raha’ astaafu kucheza soka la kulipwa.

Xtra 90 Media By Xtra 90 Media
16 Jul 2026
‘Waziri wa Raha’ astaafu kucheza soka la kulipwa.

Aliyekuwa kiungo mahiri wa Yanga SC, Mahlatse Skudu Makudubela “Waziri wa Raha”, ametangaza rasmi kustaafu soka la kulipwa, akihitimisha safari ya miaka 17 iliyosheheni mafanikio, mataji na kumbukumbu nyingi ndani na nje ya bara la Afrika.

Nyota huyo wa Afrika Kusini amewahi kuzitumikia klabu kadhaa zenye heshima kubwa zikiwemo Mamelodi Sundowns, Orlando Pirates, Chippa United, Young Africans SC, AS Vita Club na Wiliete FC. Katika kipindi hicho alifanikiwa kutwaa mataji mbalimbali, yakiwemo MTN8, Telkom Cup pamoja na ubingwa wa Ligi Kuu Tanzania Bara (NBC Premier League) akiwa na Yanga SC.

Kupitia taarifa yake ya kuaga soka, Skudu amesema kuwa safari yake ilianza mwaka 2004 katika SAFA Transnet School of Excellence kabla ya kucheza soka la kulipwa katika nchi mbalimbali kama Afrika Kusini, Jamhuri ya Czech, Georgia, Tanzania, DR Congo na Angola. Ameeleza kuwa kila klabu aliyochezea na kila uwanja aliokanyaga vimemjenga kuwa mtu na mchezaji bora.

Aidha, ametoa shukrani kwa vilabu vyote alivyovitumikia, makocha, wachezaji wenzake, madaktari, wahudumu wa vifaa pamoja na mashabiki waliomuunga mkono katika kipindi chote cha maisha yake ya soka. Amesema mchezo huo umemfundisha nidhamu, umoja na upendo, huku ukimpa fursa ya kutimiza ndoto zake.

Skudu pia ameweka wazi kuwa hataachana na soka kabisa, kwani hatua yake inayofuata ni kuingia kwenye taaluma ya ukocha. Amesema sasa ni wakati wa “kutundika daruga” na kushika filimbi, akiwa na dhamira ya kuendelea kuchangia maendeleo ya mchezo kupitia benchi la ufundi. Wakati wa kuitumikia Yanga SC, Makudubela alikuwa mmoja wa viungo waliowavutia mashabiki kutokana na ubunifu wake, uwezo wa kutengeneza nafasi na staili yake ya kipekee uwanjani, hali iliyomfanya apewe jina la utani la “Waziri wa Raha.”

Kwa kustaafu kwake, soka linaaga mmoja wa viungo wenye kipaji kikubwa waliopita katika ligi mbalimbali barani Afrika. Tunamtakia kila la heri Mahlatse “Skudu” Makudubela katika safari yake mpya ya ukocha na maisha baada ya soka.

More Stories

APR Fc yawaondosha aigles du congo kwenye caf champions league
APR Fc yawaondosha aigles du congo kwenye caf champions league
1h ago
READ MORE →
Azam Fc yaomboleza kifo cha mlinda lango U20
Azam Fc yaomboleza kifo cha mlinda lango U20
4h ago
READ MORE →
Hatuna presha kuikabili Yanga - Kocha Gaborone United
Hatuna presha kuikabili Yanga - Kocha Gaborone United
6h ago
READ MORE →
Manqoba aweka tahadhari mechi dhidi ya Gaborone United
Manqoba aweka tahadhari mechi dhidi ya Gaborone United
8h ago
READ MORE →
Rasmi: João Pedro Atwaa Tuzo Ya Mchezaji Bora Wa Mwezi Wa Agosti
Rasmi: João Pedro Atwaa Tuzo Ya Mchezaji Bora Wa Mwezi Wa Agosti
10h ago
READ MORE →
Simba inalenga hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, nusu fainali ni lengo kubwa
Simba inalenga hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, nusu fainali ni lengo kubwa
11h ago
READ MORE →
Libasse awapiga chini Max na Mwajanga, Kwenye tuzo za Mwezi.
Libasse awapiga chini Max na Mwajanga, Kwenye tuzo za Mwezi.
11h ago
READ MORE →
Fei Toto azipotezea Simba, Yanga
Fei Toto azipotezea Simba, Yanga
13h ago
READ MORE →
Xtra 90 Bets : Utabiri wa mechi 21, Septemba 11 2026
Xtra 90 Bets : Utabiri wa mechi 21, Septemba 11 2026
16h ago
READ MORE →
UEFA champions league: matokeo ya usiku
UEFA champions league: matokeo ya usiku
23h ago
READ MORE →