Klabu ya Simba imekanusha taarifa zinazozagaa mitandaoni kwamba baadhi ya mastaa wake wapo kwenye hatua za mwisho kuondoka katika kikosi hicho wakati huu wa dirisha la usajili.
Miongoni mwa wachezaji wanaotajwa kuondoka ni kiungo mshambuliaji raia wa Senegal, Libasse Gueye, ambaye amekuwa sehemu muhimu ya kikosi cha Wekundu wa Msimbazi katika msimu uliopita.





