Local,Transfer News,Singida BS, Yanga

Chukwu aitosa Singida BS, kutua Yanga

Joel JJ By Joel JJ
β€’
23 Jul 2026
Chukwu aitosa Singida BS, kutua Yanga

Kiungo mahiri wa Nigeria, Morice Chukwu, ameachana na mpango wa kuendelea kuitumikia Singida Black Stars baada ya kugomea mkataba mpya, huku akielezwa kuwa karibu kutua kwa mabingwa wa Tanzania Bara, Yanga SC.

Chukwu ambaye alikuwa sehemu muhimu ya kikosi cha Singida BS, hayupo kwenye timu hiyo inayojiandaa kushiriki michuano ya CECAFA Kagame Cup nchini Rwanda. Hatua hiyo imeongeza nguvu kwenye taarifa za kuondoka kwake baada ya kushindwa kufikia makubaliano mapya na waajiri wake.

Taarifa kutoka ndani ya uongozi wa Yanga zinaeleza kuwa klabu hiyo tayari imekamilisha hatua kubwa za kumsajili kiungo huyo mwenye uwezo wa kucheza nafasi zaidi ya moja uwanjani, ikiwemo kiungo wa kati na beki wa kati.

Kwa mujibu wa taarifa hizo, ni suala la muda tu kabla Yanga haijamtambulisha Chukwu rasmi kama mchezaji mpya wa klabu hiyo na kuanza safari yake mpya akiwa na Wananchi ambao tayari wameanza maandalizi ya msimu ujao katika kambi ya Avic Town.

Chukwu anatarajiwa kuziba pengo la Mohamed Damaro ambaye Yanga ilikuwa na mpango wa kumsajili moja kwa moja baada ya kumalizika kwa mkataba wake wa mkopo wa miezi sita. Hata hivyo, mpango huo umefutwa na Damaro kurejea Singida BS ambako bado ana mkataba.

Usajili wa Chukwu unatarajiwa kuongeza nguvu kwenye kikosi cha Yanga kutokana na uwezo wake wa kucheza nafasi mbalimbali na uzoefu wake kwenye soka la Tanzania. Mabingwa hao wanaendelea kufanya maboresho ya kikosi chao wakielekea msimu mpya wenye changamoto ndani na mashindano ya kimataifa.

More Stories

APR Fc yawaondosha aigles du congo kwenye caf champions league
APR Fc yawaondosha aigles du congo kwenye caf champions league
7h ago
READ MORE β†’
Azam Fc yaomboleza kifo cha mlinda lango U20
Azam Fc yaomboleza kifo cha mlinda lango U20
10h ago
READ MORE β†’
Hatuna presha kuikabili Yanga - Kocha Gaborone United
Hatuna presha kuikabili Yanga - Kocha Gaborone United
12h ago
READ MORE β†’
Manqoba aweka tahadhari mechi dhidi ya Gaborone United
Manqoba aweka tahadhari mechi dhidi ya Gaborone United
14h ago
READ MORE β†’
Rasmi: JoΓ£o Pedro Atwaa Tuzo Ya Mchezaji Bora Wa Mwezi Wa Agosti
Rasmi: JoΓ£o Pedro Atwaa Tuzo Ya Mchezaji Bora Wa Mwezi Wa Agosti
16h ago
READ MORE β†’
Simba inalenga hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, nusu fainali ni lengo kubwa
Simba inalenga hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, nusu fainali ni lengo kubwa
17h ago
READ MORE β†’
Libasse awapiga chini Max na Mwajanga, Kwenye tuzo za Mwezi.
Libasse awapiga chini Max na Mwajanga, Kwenye tuzo za Mwezi.
17h ago
READ MORE β†’
Fei Toto azipotezea Simba, Yanga
Fei Toto azipotezea Simba, Yanga
19h ago
READ MORE β†’
Xtra 90 Bets : Utabiri wa mechi 21, Septemba 11 2026
Xtra 90 Bets : Utabiri wa mechi 21, Septemba 11 2026
22h ago
READ MORE β†’
UEFA champions league: matokeo ya usiku
UEFA champions league: matokeo ya usiku
1d ago
READ MORE β†’