Matola afunguka maandalizi ya Simba kuikabili Coastal Union

Joel JJ By Joel JJ β€’ 26th August 2026


Matola afunguka maandalizi ya Simba kuikabili Coastal Union

Kocha Msaidizi wa Simba, Suleiman Matola, amesema kikosi hicho kimefanya maandalizi ya kutosha kuelekea mchezo wa Ligi Kuu ya Tanzania dhidi ya Coastal Union utakaopigwa kesho Alhamisi katika Uwanja wa Isamuhyo.

Akizungumza katika mkutano na waandishi wa habari kuelekea mchezo huo, Matola amekiri kuwa wanatarajia kukutana na upinzani mkali kutoka kwa Coastal Union, akisisitiza kuwa michezo kati ya timu hizo imekuwa na ushindani mkubwa.

Matola amesema licha ya Coastal Union kutokuwa na matokeo mazuri katika michezo yake ya hivi karibuni, kiwango cha uchezaji cha timu hiyo kinawafanya Simba kutarajia mchezo mgumu.

“Maandalizi yetu yanakwenda vizuri, nina imani haitakuwa mechi rahisi. Simba na Coastal Union ni timu zenye upinzani mkali kila zinapokutana.”

Ameongeza:

“Ukiwaangalia Coastal Union wamekuwa hawana matokeo mazuri lakini wamekuwa wakicheza vizuri na kuonyesha ushindani mkubwa. Hii inatufanya tuamini tutakuwa na mechi ngumu kesho.”

Hata hivyo, Matola amesema Simba imejipanga kuhakikisha inapata alama zote tatu katika mchezo huo.

“Lakini pamoja na ugumu wao, sisi tumejiandaa vyema kuhakikisha tunapata alama tatu katika mchezo wa kesho,” alisema Matola.

Matola azungumzia FVS na kadi nyekundu

Mbali na maandalizi ya mchezo huo, Matola pia amezungumzia matumizi ya FVS katika Ligi Kuu msimu huu, akieleza kuwa teknolojia hiyo imekuwa na umuhimu katika kuongeza usahihi wa maamuzi ya waamuzi.

Kocha huyo amesema Simba imechukua hatua mbalimbali katika mazoezi ili kuwajengea wachezaji umakini zaidi na kuepuka makosa yanayoweza kusababisha adhabu zaidi.

“Ni uamuzi muhimu kuleta FVS kwenye ligi yetu. Tumefanya kazi kubwa uwanja wa mazoezi ili kuongeza umakini kwa wachezaji na kuweza kuepuka yale ambayo yalikuwa hayaonekani na sasa yanaonekana,” alisema Matola.


  

More Stories

Liverpool waingia mbio za kumsajili winga wa Senegal Ismaila Sarr
Liverpool waingia mbio za kumsajili winga wa Senegal Ismaila Sarr
Today, READ MORE β†’
Rasmi: Yanga Wamkopesha Ninju Kwenda Polisi Tanzania
Rasmi: Yanga Wamkopesha Ninju Kwenda Polisi Tanzania
Today, READ MORE β†’
Matola afunguka maandalizi ya Simba kuikabili Coastal Union
Matola afunguka maandalizi ya Simba kuikabili Coastal Union
Today, READ MORE β†’
Ayyoub Bouaddi atua Manchester City kwa ada ya rekodi
Ayyoub Bouaddi atua Manchester City kwa ada ya rekodi
Today, READ MORE β†’
Xtra 90 Bets : Utabiri wa mechi 14, August 26 2026
Xtra 90 Bets : Utabiri wa mechi 14, August 26 2026
Today, READ MORE β†’
LASK, Bodo/Glimt na Sabah Fc zaandika historia UEFA Champions League.
LASK, Bodo/Glimt na Sabah Fc zaandika historia UEFA Champions League.
Today, READ MORE β†’
Bruno Fernandes Mchezaji Bora wa Mwaka EPL 2025/26 Kwa Kura za Wachezaji
Bruno Fernandes Mchezaji Bora wa Mwaka EPL 2025/26 Kwa Kura za Wachezaji
Today, READ MORE β†’
NBC Premier League: Namungo na Polisi Tanzania Zapata Ushindi.
NBC Premier League: Namungo na Polisi Tanzania Zapata Ushindi.
Today, READ MORE β†’
Xabi Alonso - Enzo Akiondoka Chelsea Sitoshangaa
Xabi Alonso - Enzo Akiondoka Chelsea Sitoshangaa
Yesterday, READ MORE β†’
NBC Premier League Leo: Michezo Miwili Yaendelea
NBC Premier League Leo: Michezo Miwili Yaendelea
Yesterday, READ MORE β†’