Paris Saint-Germain (PSG) wameepuka kipigo baada ya kufunga mabao mawili katika dakika za nyongeza na kulazimisha sare ya 2-2 dhidi ya Lille katika mchezo wa mzunguko wa pili wa Ligi Kuu ya Ufaransa.
Lille walionekana kuwa kwenye nafasi nzuri ya kupata ushindi baada ya kujenga uongozi wa mabao mawili, lakini Vitinha alifunga bao la kwanza la PSG katika dakika ya kwanza ya nyongeza kabla ya nahodha Marquinhos kusawazisha kwa kichwa katika dakika za mwisho za mchezo.
Lille walifungua bao dakika ya 21 kupitia Hakon Arnar Haraldsson, huku Olivier Giroud akihusika katika maandalizi ya mabao yote mawili ya wenyeji. Lille waliongeza bao la pili dakika ya 84 kabla PSG kufanya comeback ya dakika za mwisho.
Sare hiyo imeifanya Lille kufikisha pointi nne na kukaa kileleni mwa msimamo wa awali, wakati PSG wana pointi mbili baada ya michezo miwili na bado hawajapata ushindi katika ligi msimu huu.



