Nasreddine Nabi aachana rasmi na Raja Casablanca

Abdulrahman Said By Abdulrahman Said • 1st September 2026


Nasreddine Nabi aachana rasmi na Raja Casablanca

Kocha wa Tunisia, Nasreddine Nabi, ameondoka rasmi katika klabu ya Raja Casablanca ya Morocco baada ya wiki kadhaa za mvutano na Mkurugenzi wa Michezo wa klabu hiyo, Rogério Matias.

Mvutano huo ulihusishwa zaidi na sera za usajili, huku Nabi akidaiwa kutoridhishwa na baadhi ya wachezaji waliosajiliwa na klabu badala ya wale aliowahitaji. Pia kulikuwa na tofauti kuhusu mustakabali wa Badr Benoun, ambaye Nabi alitaka abaki katika kikosi lakini uongozi ulikuwa na mtazamo tofauti.

Nabi kupitia ujumbe wake kwenye mitandao ya kijamii amesema hakuwa na nia ya kuzua mgogoro, akisisitiza kuwa hakuna mchezaji, kocha au mtu binafsi aliye juu ya taasisi. Pia amewashukuru mashabiki wa Raja, akiwemo Ultra Eagles na Green Boys, kwa mapokezi na sapoti waliyompa wakati akiwa klabuni hapo.

Kuondoka kwa Nabi kunaongeza sura nyingine katika mabadiliko ya benchi la ufundi la Raja Casablanca, ikiwa ni kocha wa nane kuondoka tangu klabu hiyo imalize msimu bila taji chini ya Josef Zinnbauer mwaka 2024.


  

More Stories

Yanga kuanza kampeni za kimataifa na jezi mpya
Yanga kuanza kampeni za kimataifa na jezi mpya
Today, READ MORE →
Waamuzi wanne kutoka Tanzania wateuliwa na CAF kuchezesha mchezo wa Ligi ya Mabingwa Afrika
Waamuzi wanne kutoka Tanzania wateuliwa na CAF kuchezesha mchezo wa Ligi ya Mabingwa Afrika
Today, READ MORE →
Waamuzi wa Tanzania kuchezesha JS Saoura dhidi ya Horoya
Waamuzi wa Tanzania kuchezesha JS Saoura dhidi ya Horoya
Today, READ MORE →
Uwanja ndio sababu hatufungi magoli mengi : Steve Berker Kocha wa Simba
Uwanja ndio sababu hatufungi magoli mengi : Steve Berker Kocha wa Simba
Today, READ MORE →
Mashabiki wa Simba wamgusa Doumbia kwa ujumbe wa upendo
Mashabiki wa Simba wamgusa Doumbia kwa ujumbe wa upendo
Today, READ MORE →
Nasreddine Nabi aachana rasmi na Raja Casablanca
Nasreddine Nabi aachana rasmi na Raja Casablanca
Today, READ MORE →
Saka Aipa Arsenal Ushindi wa Pili Mfululizo, Clean Sheet Bado Haijavunjwa.
Saka Aipa Arsenal Ushindi wa Pili Mfululizo, Clean Sheet Bado Haijavunjwa.
Today, READ MORE →
NBC Premier League: Azam Yaibuka na Pointi Tatu licha ya Red Card.
NBC Premier League: Azam Yaibuka na Pointi Tatu licha ya Red Card.
Today, READ MORE →
Atlético Madrid Yampa Julián Álvarez Dili la €120M kwa Barcelona Januari.
Atlético Madrid Yampa Julián Álvarez Dili la €120M kwa Barcelona Januari.
Today, READ MORE →
Lionel Messi astaafu soka la kimataifa akiwa na historia isiyofutika.
Lionel Messi astaafu soka la kimataifa akiwa na historia isiyofutika.
Today, READ MORE →