Kocha Mkuu wa Simba Steve Berker ameweka wazi kutorudhishwa na uwanja wa Meja jenerali Isamuhyo akisema uwanja huo umekuwa changamoto kubwa kwa Timu yake katika kutengeneza na kufunga mabao mengi .
Berker amesema hayo apo Jana baada ya mchezo dhidi Geita Gold ambapo timu ya Simba iliibuka na Ushindi wa mabao mawili kwa sifuri, kupitia kwa viungo washambuliaji Cletous Chama na Libasse Gueye
Simba ambayo ilitangaza karibuni kufanya uwanja huo kuwa uwanja wake wa nyumbani tayari imekwisha cheza michezo miwili huku ikifunga jumla ya mabao matatu katika michezo hiyo



