Nahodha msaidizi na mlinzi wa Simba SC, Rushine De Reuck, amewatoa hofu mashabiki wa klabu hiyo, akiahidi kufanya vizuri zaidi katika msimu huu kuliko walivyofanya msimu uliopita.
De Reuck ametoa kauli hiyo wakati Simba ikielekea nchini Malawi kwa ajili ya mchezo wa mkondo wa kwanza wa Ligi ya Mabingwa Afrika, huku akisisitiza dhamira ya timu hiyo kufanya vizuri katika kampeni za kimataifa.
Simba itashuka uwanjani Jumapili dhidi ya Mighty Wanderers ya Malawi, katika mchezo unaotarajiwa kuwa na ushindani mkubwa, huku Wekundu wa Msimbazi wakilenga kupata matokeo mazuri kabla ya mchezo wa marudiano.



