Local, Normal News, Yanga, Ligi ya mabingwa afrika, Hersi, Azizi KI, Gaborone, Tanzania, Ligi kuu Bara

Yanga yazindua tawi jipya Botswana, yaahidi ubingwa wa afrika

Abdulrahman Said By Abdulrahman Said
β€’
2h ago
Yanga yazindua tawi jipya Botswana, yaahidi ubingwa wa afrika

Rais wa Yanga SC, Mhandisi Hersi Said, amesema klabu hiyo inalenga kufanya vizuri katika Ligi ya Mabingwa Afrika msimu huu, ikiwemo kufika hatua ya fainali na kuwania ubingwa wa michuano hiyo.

Akizungumza wakati wa uzinduzi wa tawi jipya la Yanga jijini Gaborone, Botswana, Hersi amesema Gaborone United ni timu nzuri, lakini Yanga imejiandaa vyema na haijaenda Botswana kwa ajili ya kushiriki tu. Amesisitiza kuwa endapo watafika fainali, dhamira yao ni kuhakikisha wanabeba kombe hilo.

Hersi pia ameeleza kuwa uzinduzi wa tawi hilo unalenga kuwapa wanachama wa Yanga wanaoishi nje ya Tanzania fursa ya kupata huduma na kutekeleza haki zao za uanachama. Amesema tawi hilo lina wanachama 63, idadi inayozidi mahitaji ya kikatiba ya wanachama 20 kwa ajili ya kuanzisha tawi.

Aidha, Rais huyo amesema tawi la Gaborone ni la 18 la Yanga lililoanzishwa nje ya Tanzania, akieleza kuwa hatua hiyo ni sehemu ya ukuaji wa chapa ya klabu na mtandao wake wa wanachama na mashabiki katika mataifa mbalimbali.

More Stories

Pacome atuma salamu Yanga kuelekea mchezo wa Gaborone united
Pacome atuma salamu Yanga kuelekea mchezo wa Gaborone united
1h ago
READ MORE β†’
Barker ataja mkakati wa ushindi Malawi
Barker ataja mkakati wa ushindi Malawi
1h ago
READ MORE β†’
Mnyama katika mtego wa Mighty Wonderers Jumapili
Mnyama katika mtego wa Mighty Wonderers Jumapili
3h ago
READ MORE β†’
Jkt tanzania na Pamba jiji kwenye vita ya alama leo
Jkt tanzania na Pamba jiji kwenye vita ya alama leo
5h ago
READ MORE β†’
Yanga mtegoni Botswana, kuikabili Gaborone United leo
Yanga mtegoni Botswana, kuikabili Gaborone United leo
7h ago
READ MORE β†’
Real Madrid na PSG zakutana na vipigo katika ligi zao.
Real Madrid na PSG zakutana na vipigo katika ligi zao.
15h ago
READ MORE β†’
Chama: Ilikuwa ngumu kucheza dhidi ya simba nikiwa na jezi ya timu nyingine
Chama: Ilikuwa ngumu kucheza dhidi ya simba nikiwa na jezi ya timu nyingine
17h ago
READ MORE β†’
Clatous Chama : Nilijutia kuondoka simba
Clatous Chama : Nilijutia kuondoka simba
17h ago
READ MORE β†’
Massanza akumbana na faini kamati ya saa 72
Massanza akumbana na faini kamati ya saa 72
1d ago
READ MORE β†’