Local, Normal News, CAFCL, Yanga, Gaborone United

Sele Gomez avuruga sherehe Gaborone United dakika za Jioni

Joel JJ By Joel JJ
β€’
1h ago
Sele Gomez avuruga sherehe Gaborone United dakika za Jioni

Yanga SC imeanza kampeni yake ya kimataifa kwa kupata sare muhimu ya bao 1-1 ugenini dhidi ya Gaborone United, katika mchezo wa mkondo wa kwanza wa hatua ya awali ya Ligi ya Mabingwa Afrika.

Yanga ilionyesha kiwango kizuri kwa kutawala mchezo kwa muda mwingi, lakini ilikumbana na ukuta mgumu wa Gaborone United ambao walitumia muda mwingi wa mchezo wakijilinda kwa wachezaji wengi.

Gaborone United ndio waliokuwa wa kwanza kupata bao dakika ya 33 kupitia mpira wa adhabu uliopigwa nje kidogo ya eneo la 18. Obry Amseb aliucheza kwa ustadi mpira huo na kuipatia timu yake uongozi wa 1-0.

Baada ya bao hilo, Yanga iliendelea kulisakama lango la wenyeji, huku Gaborone United wakionekana kuridhika zaidi na kujilinda ili kuhifadhi uongozi wao.

Hata hivyo, wakati mchezo ukielekea dakika za mwisho na wenyeji wakiamini wangeondoka na ushindi, Seleman Mwalimu 'Gomez' alivuruga sherehe hiyo kwa kufunga bao la kusawazisha dakika za lala salama.

Bao hilo lilianza na pasi ya Maxi Nzengeli iliyopenya kwenye safu ya ulinzi ya Gaborone United na kumfikia Mudathir Yahya. Mudathir hakusita, akatoa pasi ya kisigino iliyomkuta Mwalimu, ambaye alimalizia kwa ustadi na kuifanya Yanga isawazishe 1-1.

Kwa ujumla, dakika zote 90 zilitawaliwa zaidi na Yanga, huku changamoto kubwa ikiwa ni namna ya kuvunja ukuta wa Gaborone United ambao walijilinda kwa wachezaji wengi.

Sare hiyo ni matokeo muhimu kwa Yanga, ambayo sasa itakuwa na dakika 90 za nyumbani kusaka ushindi utakaoiwezesha kufuzu hatua inayofuata. Timu hiyo pia itaingia kwenye mchezo wa marudiano ikiwa na faida ya bao ililofunga ugenini.

More Stories

Highlights : Gaborone United 1-1 Yanga
Highlights : Gaborone United 1-1 Yanga
2h ago
READ MORE β†’
Pacome atuma salamu Yanga kuelekea mchezo wa Gaborone united
Pacome atuma salamu Yanga kuelekea mchezo wa Gaborone united
8h ago
READ MORE β†’
Barker ataja mkakati wa ushindi Malawi
Barker ataja mkakati wa ushindi Malawi
9h ago
READ MORE β†’
Yanga yazindua tawi jipya Botswana, yaahidi ubingwa wa afrika
Yanga yazindua tawi jipya Botswana, yaahidi ubingwa wa afrika
10h ago
READ MORE β†’
Mnyama katika mtego wa Mighty Wonderers Jumapili
Mnyama katika mtego wa Mighty Wonderers Jumapili
11h ago
READ MORE β†’
Jkt tanzania na Pamba jiji kwenye vita ya alama leo
Jkt tanzania na Pamba jiji kwenye vita ya alama leo
13h ago
READ MORE β†’
Yanga mtegoni Botswana, kuikabili Gaborone United leo
Yanga mtegoni Botswana, kuikabili Gaborone United leo
15h ago
READ MORE β†’
Real Madrid na PSG zakutana na vipigo katika ligi zao.
Real Madrid na PSG zakutana na vipigo katika ligi zao.
23h ago
READ MORE β†’
Chama: Ilikuwa ngumu kucheza dhidi ya simba nikiwa na jezi ya timu nyingine
Chama: Ilikuwa ngumu kucheza dhidi ya simba nikiwa na jezi ya timu nyingine
1d ago
READ MORE β†’