Local, Normal News, Tanzania, Barcelona, Camp nou, Afcon 2027, Kenya, Uganda

Makonda azuru Barcelona, mazungumzo ya maendeleo ya soka Tanzania yatajwa

Abdulrahman Said By Abdulrahman Said
β€’
1d ago
Makonda azuru Barcelona, mazungumzo ya maendeleo ya soka Tanzania yatajwa

Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Paul Makonda, ameanza ziara maalum nchini Hispania kwa ajili ya kufanya mazungumzo na uongozi wa klabu ya FC Barcelona, akilenga kujadili fursa za ushirikiano katika maendeleo ya soka nchini Tanzania.

Mazungumzo hayo yanahusisha maeneo mbalimbali ya maendeleo ya soka, ikiwemo ukuaji wa vipaji, maendeleo ya kiufundi, uendeshaji wa timu za taifa pamoja na kujifunza uzoefu wa Barcelona katika maandalizi ya mashindano makubwa ya soka. Tanzania ni miongoni mwa wenyeji wa AFCON 2027 pamoja na Kenya na Uganda.

Katika ziara hiyo, Makonda anaambatana na wataalamu kutoka Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Baraza la Michezo la Taifa (BMT) pamoja na Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), huku akitarajiwa pia kushuhudia mchezo wa Barcelona dhidi ya Racing Santander uliopangwa kufanyika Septemba 16, 2026.

Ziara hiyo inalenga pia kufungua fursa za kujifunza na kushirikiana na moja ya klabu kubwa duniani katika maeneo ambayo yanaweza kuchangia maendeleo ya soka la Tanzania, hususan katika malezi ya vipaji, utaalamu wa kiufundi na uendeshaji wa soka.

More Stories

Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
46m ago
READ MORE β†’
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
1h ago
READ MORE β†’
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
2h ago
READ MORE β†’
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
2h ago
READ MORE β†’
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
15h ago
READ MORE β†’
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
15h ago
READ MORE β†’
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
16h ago
READ MORE β†’
Clement Mzize arejea rasmi kikosini baada ya miezi sita nje kwa majeraha
Clement Mzize arejea rasmi kikosini baada ya miezi sita nje kwa majeraha
21h ago
READ MORE β†’
AFCON 2027 kuitangaza tanzania kama kivutio cha utalii duniani: karia
AFCON 2027 kuitangaza tanzania kama kivutio cha utalii duniani: karia
21h ago
READ MORE β†’
Ibenge asifu ubora wa simba, huku akitoa sababu za rotation zake
Ibenge asifu ubora wa simba, huku akitoa sababu za rotation zake
22h ago
READ MORE β†’