Local, Normal News, Tanzania, TFF, Makonda, Sandaland, Taifa stars

Wizara kuunda kamati kuchunguza mkataba wa jezi timu za taifa

Abdulrahman Said By Abdulrahman Said
1h ago
Wizara kuunda kamati kuchunguza mkataba wa jezi timu za taifa

Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo chini ya Waziri Paul Makonda imepanga kuunda kamati maalumu ya kuchunguza mkataba wa mzabuni wa jezi za timu za taifa, huku ikitaka kubaini manufaa ya mkataba huo kwa timu zinazowakilisha Tanzania.

Hatua hiyo imekuja baada ya kuzuka sintofahamu kuhusu jezi mpya za Timu ya Taifa ya Tanzania, Taifa Stars, huku Wizara ikitaka kupata ufafanuzi kuhusu mkataba huo na namna unavyowanufaisha timu za taifa ambazo zimekuwa zikigharamiwa na Serikali.

Kwa mujibu wa taarifa ya Wizara, uchunguzi huo utalenga kupitia mkataba huo na kubaini iwapo masharti yake yanaendana na maslahi ya timu za taifa pamoja na uwekezaji unaofanywa na Serikali katika kuzigharamia timu hizo.

Wizara pia imeweka wazi kuwa suala hilo linahitaji kufanyiwa uchunguzi ili kupata uelewa wa kina kuhusu mkataba wa mzabuni huyo na manufaa yanayopatikana kwa upande wa timu za taifa.

More Stories

Kocha Dimitar Pantev ateuliwa kuwa kocha mpya wa Richard Bay.
Kocha Dimitar Pantev ateuliwa kuwa kocha mpya wa Richard Bay.
6m ago
READ MORE →
Sandaland kuchukua hatua kufuatia kauli za Makonda juu ya jezi za Taifa stars
Sandaland kuchukua hatua kufuatia kauli za Makonda juu ya jezi za Taifa stars
12m ago
READ MORE →
Tuchel awarejesha Trent na Palmer kikosi cha England
Tuchel awarejesha Trent na Palmer kikosi cha England
1h ago
READ MORE →
Pyramids ya mokwena haishikiki misri, yaandelea kuongoza msimamo
Pyramids ya mokwena haishikiki misri, yaandelea kuongoza msimamo
3h ago
READ MORE →
EPL kuendelea leo kwa dabi ya London kati ya Brentford dhidi ya Chelsea
EPL kuendelea leo kwa dabi ya London kati ya Brentford dhidi ya Chelsea
4h ago
READ MORE →
Yanga yapambana kuondoa kadi nyekundu ya Aziz Ki kabla ya derby ya simba
Yanga yapambana kuondoa kadi nyekundu ya Aziz Ki kabla ya derby ya simba
6h ago
READ MORE →
Wamebaki wababe wawili tu wasiofungika Ligi Kuu
Wamebaki wababe wawili tu wasiofungika Ligi Kuu
1d ago
READ MORE →
Afcon haiwezi kuondoka Tanzania, Kenya na Uganda : Motsepe
Afcon haiwezi kuondoka Tanzania, Kenya na Uganda : Motsepe
1d ago
READ MORE →
BREAKING: Tajiri wa Chelsea Boehly ang’atuka kwenye klabu
BREAKING: Tajiri wa Chelsea Boehly ang’atuka kwenye klabu
1d ago
READ MORE →